Headlines News :

Home » , , , , » BOB JUNIOR AKANA KUWA NA TABIA ZA KISHOGA

BOB JUNIOR AKANA KUWA NA TABIA ZA KISHOGA

Written By Unknown on Friday, November 23, 2012 | 2:49 PM


Alisema mara baada ya kuitoa video ya wimbo wake huo akiwa anakata sana mauno, watu walikuwa wakimpigia simu, wengine wakimtumia meseji kwamba, anaonekana ni ‘chakra’ maana anayaweza sana mauno.

“Watu wanasema mimi ni shoga, lakini si kweli. Kisa kilianzia kwenye ule wimbo wangu wa Oyoyo. Unajua katika video ya ule wimbo nilikata sana mauno, watu wakaamini mimi shoga.
“Wengine walikuwa wakinitumia hata meseji wakiamini hivyo. Kwa hiyo sababu kubwa ni ile video tu, watu wana mambo ya ajabu sana,” alisema Bob Junior huku watu  alioongozana nao usiku huo wakitingisha vichwa kukubaliana naye.

Ishu ya Bob Junior kuonekana ni chakra pia iliwahi kusababisha amfikishe kortini kwenye Mahakama ya Mwanzo Kinondoni, Miss Tanzania 2006, Wema Sepetu akidaiwa kumtukana msanii huyo matusi ya nguoni likiwemo hilo la ushoga.

Katika kesi hiyo iliyofikishwa kwenye mahakama hiyo kwa mara ya kwanza Mei 4, 2011 na kusikilizwa na Hakimu Mfawidhi Mariam Masamalo, Wema alihukumiwa kulipa faini ya shilingi 40,000 au kwenda jela miezi 6 ambapo alifanikiwa kulipa.
Share this article :

0 comments:

Speak up your mind

Tell us what you're thinking... !

 
Deigned by: Bongo Blog Designers | Bloggerized by | Tryphone Chasama Jr
Proudly powered by Bongo Blog Designers
Copyright © 2011. THINK BIG - All Rights Reserved
Template Design by Creating Website Published by Mas Template